Dunia ya Leo inahitaji jamii inayochangamkia fursa za maendeleo katika
Nyanja mbalimbali za kiuchumi,kijamii,kiroho,kitaaluma nk Katika kuzingatia
hilo Kanisa la Waadventista wa Sabato limedhamiria kuihubiri injili
ya kweli kupitia vyombo vya Habari hasa Radio na TV.Ni katika Muktadha huo
Mwenyekiti wa Kanisa Hili katika jimbo kuu la Kaskazini mwa
Tanzania Mch na Dr Godwin Lekundayo Alishiriki kuchangia Vituo vya kanisa hilo
MORNING STAR RADIO na MORNING STAR TV.
Tukio hilo lilikusanya watu kutoka ndani na Nje ya Jiji la Arusha.
Aidha Dr Godwin Lekundayo aliwaasa watu wote kutambua kuwa ulimwengu wa
sasa unahitajia jamii yenye uelewa mpana juu ya Kuongezeka kwa Maarifa pia kuyatumia
vema katika kuusambaza ujumbe mwema.
Katika habari hii utaona picha za Matukio mbalimbali yaliyojiri siku hiyo katika
viwanja vya Kanisa la Waadventista wa Sabato Burka JIjini Arusha.